Vichwa vya Habari
Makala Maalum
Haki za binadamu
Hali katika vituo vya rumande nchini Ufilipino, ambayo imeelezwa kuwa “si ya kibinadamu” na mmoja wa majaji wa mahakama ya juu nchini humo, inatarajiwa kuboreka kwa kasi wakati taifa hilo la Kusini Mashariki mwa Asia likielekea katika kupitisha sheria zinazozingatia haki za binadamu na utu wa wafungwa na kupendekeza kiwango cha chini cha matibabu katika vituo vyote vya rumande.
Habari kwa Picha
Harakati za kusaka usalama huko Gaza
Wengi wa wananchi wa Gaza milioni 2.3 wanakimbia ghasia zinazozidi kaskazini na Kusini mwa Gaza kutokana na vita ambayo sasa ina miezi saba na ambayo imesababisha vifo vya wapalestina 36,000 na kuwaacha wengine katika njaa huku wengine wakiwa wamefukiwa kwenye vifusi katika maeneo yaliyo zingirwa.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limeiitisha mjadala wa wazi kuhusu mgogoro unaoendelea Gaza, ambao unazidi kughubikwa na madhila makubwa yanayochangiwa na kuporomoka kabisa kwa ko mfumo wa sheria na utulivu na mfumo wa kibinadamu uko ukingoni kuporomoka kabisa.
Amani na Usalama
Hali ya kibinadamu inaendelea kuwa mbaya Gaza huku leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yakiripoti kuendelea kwa mashambulizi yanayokatili maisha ya watu na kuathiri miundombinu ya raia kuanzia kwenye shule hadi vituo vya afya huku maelfu ya watu wakiendelea kukabiliwa na ukosefu wa huduma za msingi ikiwemo afya, makazi, maji na chakula kadri vita vinavyoendelea.