Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Tabianchi na mazingira

Profesa Ruth Wanjau, ni mtafiti na mkemia kutoka Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya. Wamebuni mbolea inayotengenezwa na taka za plastiki. Mbolea hii inafaa kwenye maeneo yenye ukame.
UN News/Assumpta Massoi

Mbolea itengenezwayo kwa taka za plastiki ni mkombozi maeneo ya ukame- Profesa Ruth

Kutana na Profesa Ruth Wanjau, mbobezi wa kemia katika Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya, ambaye andiko lake la dhahania kuhusu mbolea itengenezwayo kwa kutumia taka za plastiki lilimkutanisha na wajasiriamali na wawekezaji kwenye Jukwaa la nne la kimataifa la uwekezaji kwa wajasiriamali, WEIF 2024  huko Manama nchini Bahrain, mwezi Mei mwaka huu.

Sauti
4'39"
Vidonge na vidonge visivyo vya kiasili. (Maktaba)
© Unsplash/Roberto Sorin

 WHO yatoa mwongozo wa kudhibiti uchafuzi unaosababishwa na watengenezaji wa viuavijasumu

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limechapisha mwongozo wake wa kwanza kabisa kuhusu uchafuzi wa viuavijasumu unaotokana na  uzalishaji viwandani. Mwongozo huu unaohusu usimamizi wa maji taka na taka ngumu katika uzalishaji wa viuavijasumu unaangazia changamoto hii iliyopuuzwa huku dunia ikisubiri Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) kuhusu vijidudu au vijiumbe maradhi vyenye usugu kwa dawa za viua vijiumbe maradhi, au AMR unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Septemba 2024 

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP nchini Tanzania linashirikiana na vijana wakulima kuwawezesha kuondokanana kilimo cha mazoea na badala yake kiwe cha kisasa na kinachohimili mabadiliko ya nchi.
WFP Tanzania

WFP Tanzania yajengea uwezo wakulima vijana

Mradi wa Vijana Kilimo Biashara (VKB) unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani (WFP) nchini Tanzania unawapatia vijana wakulima wadogo ujuzi na rasilimali zinazohitajika ili kuboresha uzalishaji wa chakula na kujenga uchumi endelevu wakati huu ambao madhara ya El niño yanayosabisha ukame na mafuriko yamekuwa dhahiri. 

Sauti
1'50"
Januari 29 2019 Mynmar, watoto wakicheza katika kambi ya wakimbizi wa ndani Sittwe mji mkuu wa jimbo la Rakhine.
© UNICEF/Nyan Zay Htet

WFP kufikia jamii zilizoathiriwa na mafuriko Myanmar

Wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesema kwamba timu za misaada zimeanza kusambaza misaada ya dharura kwa familia zilizoathiriwa na mvua za masika katika Delta ya Ayeyarwady huko Myanmar na kusema kuwa takribani watu 500,000 katika eneo muhimu linalolimwa mpunga wanaweza kuathirika.

Mama akiwa na mwanae kwenye kifusi cha nyumba baada ya kusombwa na kimbunga Idai mwaka 2019.
WFP/Deborah Nguyen

Msumbiji yazindua mpango wa utoaji mapema wa maonyo ya majanga kwa wote

Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi, amezindua mpango wa kitaifa wa kuhakikisha kila mtu anapata Maonyo ya Mapema kuhusu hali ya hewa, EW4All ifikapo mwishoni mwa mwaka 2027 huku akitangaza uwekezaji mpya muhimu ili kuboresha uchunguzi wa kimsingi wa hali ya hewa, uzinduzi uliofanyika katika hafla ya ngazi ya mawaziri iliyofanyika katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo. 

Audio Duration
1'59"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (kushoto) akutana na mwanajamii wa eneo hilo kutoka Lalomanu, Samoa.
United Nations/Kiara Worth

Katibu Mkuu UN ahimiza haki ya mataifa ya Pasifiki katika suala la tabianchi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa ziarani Samoa, visiwa vilivyoko huko baharí ya Pasifiki akizungumza na waandishi wa habari amelisifu taifa hilo kwa uimara wake wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ongezeko la kina cha baharí, licha ya ukata utokanao na kiwango kidogo cha ufadhili kwa tabianchi. Amesema dunia itumie mikutano ya mwezi ujao kuchagiza marekebisho ya taasisi za fedha duniani ili ziongeze ufadhili.