Sasa maandamano na kujieleza kwa uhuru ni ruhusa Bangladesh - Yunus
Mshauri Mkuu wa serikali ya mpito nchini Bangladesh, Muhammad Yunus amehutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA79 jijini New York, Marekani na kueleza mambo ya msingi wanayofanya hivi sasa ili kurejesha utawala wa haki na wa amani nchini humo baada ya maandamano yaliyosababisha Waziri Mkuu kukimbia nchi.