Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Wahamiaji na Wakimbizi

Wanawake katika kambi ya wakimbizi ya ndani ya Rusayo iliyoko jimbo la Kivu Kaskazini, mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
UNHCR Video

Suluhu ya janga la kibinadamu DRC ni amani: UNHCR

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, imesalia katika mgogoro kwa miaka mingi, hali ambayo imewasababishia raia mateso ya hali ya juu zaidi yakiwemo mauaji, utekaji nyara, na kuteketezwa kwa nyumbaa zao. Mapigano hayo pia yamewafungisha viragozaidi ya watu milioni 6.4 nchini humo, na kulazimisha familia kutafuta usalama katika makazi ya muda yaliyojaa pomoni. 

Sauti
2'23"
Familia zinaishi katika maeneo ya wakimbizi wa ndani katika maeneo mbalimbali huko Port-au-Prince.
© IOM

IOM yatoa ripoti ya ongezeko la wakimbizi wa ndani nchini Haiti

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limeripoti kuwa zaidi ya watu 700,000, nusu yao wakiwa watoto, wamekimbia makazi yao ndani ya Haiti kufuatia kuongezeka kwa machafuko. Ripoti hiyo mpya inaonesha ongezeko la asilimia 22 la wakimbizi wa ndani tangu mwezi Juni, huku hali ya kibinadamu nchini humo ikiendelea kuzorota.

Watu wanaokimbia mashambulizi nchini Lebanon wakifika kwenye mpaka na Syria.
© UNICEF/Rami Nader

Muhtasari wa habari - Lebanon, Sudan, Haiti

Huko Mashariki ya Kati, nchini Lebanon hali inaendelea kuwa tete amesema mratibu maalum wa Umoja wa mataifa nchini humo Jeanine Hennis Plasschaert. Kupiti ukurasa wake wa mtandao wa X amesema umekuwa usiku mwingine wa kutoka kulala mjini Beiruti milipuko ikighubika mji huo bila tahadhari, raia  wakikumbwa na taharuki bila kujua mustakbali wao.