Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Masuala ya UM

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ( Kutoka makataba)
UN Photo/Eskinder Debebe

Guterres atoa wito wa ulinzi kwa walinda amani baada ya IDF kukiuka msimamo wa UN Lebanon

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Antonio Guterres leo Jumapili amesisitiza kwamba ulinzi na usalama wa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na mali za Umoja wa Mataifa lazima uhakikishwe, kufuatia uvunjaji wa makusudi wa sheria katika kituo cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani uliofanywa na magari ya kivita ya jeshi la Israel IDF kusini mwa Lebanon.

Marafiki watatu katika eneo la Afar nchini Ethiopia ambao wanapigania haki za wasichana na hatua dhidi ya ukeketaji wa wanawake (FGM) na ukatili wa kijinsia.
© UNICEF/Martha Tadesse

Ni wakati muafaka sisi kuwasikiliza wasichana – Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa

Ikiwa le oni Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa kuwapa sikio watoto wa kike akianza ujumbe wake mahususi kwa ajili ya siku hii akisema uwezo wa wasichana zaidi ya bilioni 1.1 duniani hauna kikomo lakini tunapokaribia tarehe mwaka 2030, wa mwisho kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu, ulimwengu unaendelea kuwaangusha wasichana.

Sauti
1'45"
Mbusa Thasikalyo, mkazi wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya  Kidemokrasia ya Congo, DRC.
UN News/George Musubao

Hatuhitaji chochote zaidi ya amani DRC, asema Thasikalyo (60)

"Mimi ni Mbusa Thasikalyo nina miaka 60. Zamani kabla ya vita hii hatukuishi kimaskini. Tulikula chakula kutoka mazao ya shambani tena kizuri sana. Tulikula nyama lakini kwa sababu ya vita, sasa tunahangaika. Huyu ni mkazi wa Goma, mashariki kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisimulia madhila ya wazee, leo siku ya wazee duniani.

Mwakilishi wa Kudumu wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Rwamucyo Ernest akihutubia Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.
UN Photo/Loey Felipe

UNGA79 Rwanda: Kurekebisha taasisi za kimataifa za fedha na Baraza la Usalama ni muhimu sana

Mwakilishi wa Kudumu wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa, Balozi Rwamucyo Ernest akihutubia Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Septemba 30, pamoja na kusisitiza masuala mengine muhimu kama ushirikiano wa kimataifa, amesisitiza kufanyia mageuzi mashirika ya kimataifa ya fedha na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ili kuhakikisha uwakilishi wa haki, kukuza kuaminiana miongoni mwa mataifa, na kukabiliana vilivyo na changamoto za kisasa, kama vile kuyumba kwa uchumi, mabadiliko ya tabianchi na migogoro.