Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Wanawake

Ulinzi kwa programu lengwa la usalama mtandaoni, vikundi vya mawasiliano mtandaoni na majukwaa ya mitandao ya kijamii ili kuzuia unyanyasaji wa kingono mitandaoni.
© UNICEF/Ueslei Marcel

Watoto wanaokabiliwa na hatari kubwa zaidi ya unyanyasaji na unyonyaji wa kingono kutokana na matumizi mabaya ya teknolojia

Vitendo vya unyanyasaji na unyonyaji wa kingono dhidi ya watoto vimeongezeka katika mazingira ya kidijitali, huku zaidi ya watoto milioni 300 kwa mwaka wakikadiriwa kuwa waathiriwa wa vitendo hivyo mtandaoni, anasema Mama Fatima Singhateh ambaye ni Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na unyanyasaji wa kingono wa watoto.

Josephine Telo, anayeketi, anazungumza na Consolata Aleper, ambaye hufanya mikutano na manusura wa ukeketaji na kujitahidi kukomesha vitendo vya ukeketaji kwa jamii. Dadake Bi Telo alifariki wakati wa kujifungua kwa sababu ya ukeketaji.
© ActionAid International Uganda

Ukeketaji wa wanawake unasababisha vifo wakati wa kujifungua, janga linaloweza kuzuilika: Jamii Uganda

Josephine Telo, ambaye alipoteza dada yake katika Wilaya ya Amudat, Uganda, aliliambia kundi la wanawake waliopona baada ukeketaji kwamba, "dada yangu hakupaswa kufariki jinsi alivyofariki. Hii ilikuwa ni desturi." Anaongeza, akimaanisha ukeketaji wa sehemu za siri za mwanamke au msichana bila sababu za kiafya, uliosababisha kifo cha dada yake.

Liz akibeba mkoba wa ukili maalum unaotengezwa na wanawake wa Eswatini.
UN News/Thelma Mwadzaya

Ukombozi wa mwanamke ni ukombozi jamii nzima: Mwanaharakati Liz Ogumbo

Tukielekea katika mkutano wa Zama Zijazo utakaofanyika mwishoni mwa wiki hii na kisha mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa mataifa UNGA79 yote ikifanyika hapa New York, Marekani ikiangazia mchakato wa usongeshaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDG’s, tunakwenda Nairobi Kenya ambako mwandishi wetu Thelma Mwadzaya amepata fursa ya kuzungumza na mwanamuziki nyota, mjasiriamali, mlimbwende na mwanaharakati wa haki za wanawake Lizi Ogumbo kuhusu mchango wake kama kijana katika kusongesha malengo hayo ya Umoja wa Mataifa katika jamii yake hususan lengo namba 5 la usawa wa kijinsia.