Wewe Quotes

Quotes tagged as "wewe" Showing 1-13 of 13
Enock Maregesi
“Mtu akikushauri kufanya kitu ambacho ni kinyume na takdiri ('destiny') ya maisha yako, hata kama huyo mtu hana nia mbaya na wewe, sema 'hapana' kwa hiyo 'ndiyo' yake.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiua mtu bila kumwambia kwa nini unamuua anaweza kujua umemuua kwa kumwonea. Akijua umemuua kwa kumwonea roho yake inaweza kukusumbua wewe na familia yako maisha yenu yote. Makachero wa EAC wana leseni ya kuua. Lakini si kuua ovyo kama James Bond. Kila wanayemuua lazima waandike ripoti kwa nini wamemuua. Kachero wa EAC akiua mtu, kwa makosa, kwa bahati mbaya, atalindwa na Mwenyezi Mungu. Atalindwa na Tambiko la Tume ya Dunia.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mimi na wewe na vitu vyote ulimwenguni ni wazito kwa sababu ya 'Higgs Boson', inayojulikana pia kama 'The God’s Particle'. Wanasayansi wa CERN wamekuwa wakiitafuta 'higgs' (iliyojificha ndani ya 'higgs field') kwa zaidi ya miaka hamsini sasa, kwa bajeti ya pauni za Uingereza bilioni sita. Chembe ya 'higgs' ikipatikana itawajulisha wanasayansi jinsi ulimwengu unavyofanya kazi na jinsi ulivyoumbwa, na jibu la kitendawili cha 'Standard Model' litapatikana.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Hufanani na yoyote katika dunia hii. Unafanana na wewe mwenyewe. Usimdharau mtu, humjui!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu alikupa vipaji ili uwanufaishe wengine na si kujinufaisha mwenyewe, na aliwapa wengine vipaji ili kukunufaisha wewe na si kujinufaisha wenyewe, kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya katika dunia yetu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Maskini hajali wewe ni nani. Anajali utu ndani ya moyo wako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kwa nini watu wana kawaida ya kuona thamani ya mtu baada ya mtu kufariki? Kwa nini watu wana kawaida ya kuona thamani ya pumzi katika kipindi ambacho mtu hana uwezo tena wa kuvuta hewa? Nini thamani ya pumzi? Thamani ya pumzi ni kukufanya uwe wewe na si udongo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukifanya maamuzi kubaliana na matatizo yake yote. Fanya kile ulichosema utafanya, hata kama sehemu ya kile ulichosema utafanya uliinukuu kutoka kwa wengine, hata kama watu hawatakubaliana na wewe.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukila kiapo fanya kile ulichoahidi katika kiapo, si kinyume chake hata kidogo, hata kama dunia haitakubaliana na wewe.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wewe na rais wa nchi: Wewe unajua mambo ya mtaa. Rais wa nchi anajua mambo ya nchi. Anayejua mambo usiyoyajua ni wa kuogopa kama ukoma.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Unapofikia hatua ya kuwa na kila kitu katika maisha, unapokuwa umefanya kila kitu ulichotamani kufanya katika maisha, unakuwa na bahari nzima ndani ya tone ambalo ni wewe. Unaridhika. Wewe si tone tena ndani ya bahari, wewe ni bahari ndani ya tone. Kinachobaki baada ya hapo ni kusaidia jamii iliyosaidia kukulea ulipokuwa mdogo, kuacha alama katika dunia kabla na baada ya wewe kuondoka, bila kujali watu watasema nini juu ya maisha yako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mungu anataka nini zaidi kutoka kwako? Anakutaka wewe.”
Enock Maregesi
tags: god, mungu, wewe, you

Enock Maregesi
“Watu wote ni wa Mungu, watu ni matatizo. Wewe huna mtu, lakini bado unapambana na Mungu kuhusu watu.”
Enock Maregesi